Kifafa ni hitilafu fulani inayotokea kwenye mfumo wa ubongo, ambapo shughuli za ubongo zinakuwa isivyo kawaida, na kusababisha degedege au hali au hisia fulani zisizo za kawaida, na wakati mwingine kupoteza ufahamu.

Dalili za kifafa, kama degedege, zinaweza kutofautiana sana na aina ya kifafa

  • Kutoa/ kukodoa/ kuchezesha kope za macho kwa sekunde chache;
  • Kukakamaa au kutetemeka mwili mzima;
  • Kupoteza fahamu kwa dakika/sekunde chache;
  • Viungo kukamaa;
  • Kushindwa kudhibiti viungo;
  • Kukamaa vidole vya mikono au miguu.