Hapana. Mara nyingi mtu anapoanguka, hupoteza fahamu, na kupata degedege, tunapata hofu kumsaidia kwa sababu tunadhani inaweza kuwa kitu hatarishi na cha kuambukiza. Lakini hii si kweli hata kidogo.

Tafiti za kisayansi zinathibitisha kwamba mtu mwenye kifafa au anayepata degedege, hawezi kumuambukiza mtu mwingine. Tunapaswa kumsaidia ili arejee katika hali yake ya kawaida haraka iwezekanavyo.

Huwezi kuambukizwa kifafa kwa kugusa mate ya mtu aliyepata degedege.
Kifafa ni ugonjwa unaohusiana na itilafu fulani kwenye mfumo wa ubongo na degedege ni mojawapo ya dalili zake.