Mtu anapopatwa na degedege kwa mara ya kwanza, mara nyingi wanafamilia hutafuta mganga wa kienyeji au kupiga ramri ili kujua inatokana na nguvu za giza au kutupiwa jini, roho za mizimu au sababu nyinginezo zisizo za kawaida. Mara zote familia hutumia gharama kubwa.